Tuesday, September 02, 2014
|
Usiku wa jana klabu ya Manchester United
ilikamilisha usajili wa mshambuliaji wa
kimataifa wa Colombia, Radamel Falcao kwa
mkopo.
Falcao ambaye alikuwa akiwindwa na vilabu
vya Arsenal na Man City amejiunga na Man U
akitokea klabu ya Monaco ambayo alijiunga
nayo akitokea Atletico Madrid.
Usajili wa mchezaji umezungumzia na watu
wengi mmoja wao ni mchezaji bora wa ulaya
na dunia – Cristiano Ronaldo.
Akiongea jijini Madrid Ronaldo alisema:
‘Falcao ni mchezaji mzuri sana, nadhani
Manchester United wamefanya jambo zuri
kumsajili. Sidhani kabisa kama ni mchezaji
asiyewafaa, ni mchezaji wa daraja la dunia na
hivyo naamini huu usajili mzuri.” |
0 comments:
Post a Comment