Thursday, August 28, 2014

‘ HUU NDIYO UBORA WA KWANZA WA YANGA SC’

Na Baraka Mbolembole, Dar es Salaam, Tayari, Yanga SC imecheza michezo miwili ya kujiandaa na msimu mpya wa ligi kuu ya kandanda Tanzania Bara ambayo inataraji kuanza kutimua vumbi lake, 20 Septemba.IKiwa katika wiki ya pili ya michezo yote miwili dhidi ya timu za Chipukizi ya Pemba ambayo waliichapa kwa bao 1-0 lililofungwa na mshambulizi mpya, Geilson Santos ‘ Jaja’. Mchezo wa pili timu hiyo ilishinda kwa mabao 2-0 dhidi ya Shanghani FC ya Unguja Haruna Niyonzima amerejea katika kiwango chake cha juu na mchezaji huyo wa kimataifa wa Rwanda tayari ameonekana ‘ muhimili wa sehemu ya kiungo’ kutokana na uwezo wake wa kumiliki mpira kwa muda mrefu bila kuupoteza na kuchezesha timu kwa pasi za uhakika. Maximo anaonekana kutafuta mchezaji ambaye atacheza nafasi ya kiungo wa chini-namba sita. Mbuyu Twite amekuwa akichezeshwa katika nafasi hiyo na hajamuangusha mwalimu wake. Salum Telela anaonekana kuyashinda majeraha na mchezaji huyo wa nafasi ya kiungo anaweza kurudishwa nyuma zaidi katika nafasi ya beki wa kulia. Telela amechezshwa katika nafasi ya ulinzi katika michezo iliyopita ili kupisha vipaji zaidi katika nafasi ya kiungo. Nguvu na Twite zimefanya, Niyonzima kucheza kwa uhuru mkubwa katika eneo la mashambulizi, huku akisaidiwa na SAimon Msuva, Mrisho Ngassa, na Andrey Coutinho. Maximo yupo katika wakati mgumu bila shaka, kwa sababu wachezaji wote wameonyesha viwango vya juu katika maandalizi Yanga watakuwa timu yenye kasi msimu ujao, tofauti na ilivyozoeleka kwa sababu wachezaji ambao Maximo anao katika nafasi ya kiungo wote ni wenye kasi, wajanja, na watulivu hata pale mpira unapokuwa ukimilikiwa na wachezaji wa timu pinzani. Yanga wapo katika mchakato wa kutafuta mechi zaidi za kirafiki na habari zilizopo ni kwamba wanafanya mipango ya kucheza na timu za St. George ya Ethiopia, Gor Mahia ya Kenya au Zesco ya Zambia, kama watapata michezo walau miwili dhidi ya timu hizo itakuwa na faida kubwa kwa mwalimu Maximo ambaye hawezi kusema moja kwa moja kuwa tayari timu yake imeimarika kwa kuzifunga timu hizo za madaraja ya chini huko Zanzibar. Mechi hizo zinawezekana kumsaidia Maximo kujua wachezaji wake wameiva namna gani katika suala la uvumilivu, mbinu, na ufundi wanapokutana na timu ngumu, na anaweza kuitimia mechi ya Ngao ya Jamii dhidi ya Azam FC kupima kikosi chake cha kwanza. Maximo anaitengeneza Yanga kwa kutumia wachezaji wa nafasi ya kiungo, kwani amekuwa akiwachezesha viungo watano na mshambulizi mmoja katika michezo ya kirafiki. Kwa nini asifanye hivyo wakati anao wachezaji wengi wenye maarifa binafasi ya ufungaji . Alipokuwa kocha wa Taifa Stars, Maximo alikuwa akipendelea zaidi kutimia mfumo wa 4-5-1 kwa lengo la kudhibiti mechi na kutafauta ushindi wa aina yoyote, alipata wakati mgumu kutokana na kukosa wachezaji wazuri katika eneo la katikati ya uwanja na sehemu ya mashambulizi kutokana na kukosa wachezaji sahihi wa kucheza katika mfumo huo. Mfumo huo ameuleta Yanga . Niyonzima alikuwa akitumika zaidi kama kiungo mchezesha timu akitokea upande wa kushoto na kuingia hadi katikati ya uwanja chini ya makocha Ernie Brants na Hans Van Der Pluijm, ila atarudishwa katika eneo la kati kwa sababu, Ngassa Coutinho wanauwezo wa kutimiza majukumu hayo. Msuva anacheza upande mmoja tu, upande wa kulia, faida kubwa kutoka kwa kiungo huyo ni kucheza soka la kupanda na kushuka, huku akitengeneza mabao kwa mipira ya krosi, na wakati mwingine akifunga mwenyewe, Coutinho anacheza kushoto zaidi, ni mwepesi na ana kasi. Ngassa ana uwezo wa kucheza kila upande sehemu ya mashambulizi, na Maximo amekuwa akimtumia zaidi kama mshambulizi wa pili akicheza nyuma ya Jaja. Kwa maana hiyo sehemu ya kiungo ya Yanga itakuwa na wachezaji wa kubadilika badilika katika uchezaji wao uwanjani. Timu nyingi zipata wakati mgumu dhidi ya Yanga, kiufundi wanatakiwa kuongeza umakini na namna ya kulazimisha matokeo wakati mechi inapokuwa ngumu huku wakicheza katika utulivu wao. Kama unataka kuifunga Yanga SC msimu ujao jipange vizuri kuthibiti eneo lao la kiungo.

Habari zingine  BOFYA HAPA 


Posted via Blogaway

0 comments:

Post a Comment