| UVUMI kwamba uongozi wa Simba ulikuwa na
mpango wa kumtema straika namba moja,
Mrundi Amissi Tambwe, ili kumpisha Mganda
Emmanuel Okwi, jana ulizua balaa kubwa baada
ya baadhi ya mashabiki kutaka kuandamana
Mtaa wa Msimbazi, Kariakoo, jijini Dar es
Salaam kupinga, kabla ya uongozi kuzima
mambo.
Uvumi huo ulianza baada ya kudaiwa kwamba
kocha Patrick Phiri amewaambia viongozi
kwamba Mrundi mwingine, Pierre Kwizera na
Okwi wanatosha katika safu yake ya mbele.
Mapenzi ya mashabiki hao kwa Tambwe,
yamejengwa na kiwango alichokionyesha
straika huyo tangu alipotua klabuni hapo
ambapo msimu uliopita ndiye aliyekuwa
Mfungaji Bora wa Ligi Kuu Bara kwa kufunga
mabao 19.
Hadi tulipokuwa tunakwenda mitamboni jana
usiku huku usajili ukiwa katika dakika za lala
salama, Simba ilikuwa katika mazungumzoa na
mabeki, Salum Salim Mbonde, wa Mtibwa na
Juma Nyosso (huru) ili kumpata mmoja wao
kuziba nafasi ya Mkenya, Donald Mosoti,
ambaye ameomba kuachwa ili akacheze soka
Qatar.
Lakini Mwanaspoti linajua kwamba viongozi
hao walikuwa wamewekeza akili zao kwa
Mbonde kuliko Nyosso ambaye hata kocha
Phiri anamkubali.credit mwanaspoti |
0 comments:
Post a Comment