Wednesday, August 27, 2014

VAN GAAL HUWEZI KUPIKA CHAPATI KWA UNGA WA MUHOGO

Tunamshukuru aliyeleta wazo la kila kata kuwa na shule ya sekondari.Shule hizi kwa kiasi zimesaidia kufuta ujinga kwa walio wengi.Asilimia kubwa ya wanaomaliza shule za msingi wanapata nafasi za kuingia kidato cha kwanza tofauti na enzi zile za mwalimu na mzee wa ruksa.Heri nusu shari kuliko shari kamili,Ingawa shule hizi zina walakini lakini mchango wake kwenye jamii unaonekana.Tofauti ya sasa na zamani inaonekana kupitia shule hizi.Wengi hawajaelimika ila wamepunguza shari kwa kufuta ujinga.Wengi wao angalau wanajua kujieleza kwa lugha ya chakula,Pia wengi wanajua ukichanganya hydrogen na oxygen unapata maji,ukichukua sodium na chlorine unapata chumvi na ukitaka kupata chumvi na maji kwa pamoja ni lazima uchanganye acid na base. Hi ndio tunaita chemistry (kemia), kwa ufupi kemia ni masomo ya atomi na mkusanyo wa atomi kuwa molyekuli.Yaani hizo atomi ukizichanganya utapata kitu kizima kinachoitwa molyekuli,Hata ndugu zangu wajenzi wanajua ili upate zege lazima uchanganye ingredients(vitu vinavyounda zege),Ili upate zege lazima uchanganye maji, kokoto,mchanga na simenti kwa viwango maalumu. Kwenye soka tumekuwa tukitumia maneno kama chemistry (kemia) huku wengi tukiwa hatujui chimbuko lake.Mchezaji ndio atomi yenyewe na timu ndio molyekuli.Kitendo cha kuwaunganisha wachezaji katika timu moja na wachezaji hao kuungana katika mfumo husika ndio tunaita chemistry (kemia).Kocha anaposhindwa kupata wachezaji husika kwenye mfumo husika hapo ndipo tunasema kashindwa kutengeneza chemistry kwenye timu. Kocha wa manchester united Louis van gaal kama hakukimbia somo la chemistry basi anataka kutuonyesha staili mpya ya kupika chapati kwa unga wa muhogo.Van gaal amethubutu kutengeneza molyekuli ya 3-5-2 lakini amekosa atomi husika za kutengeneza chemistry.Watu wa mpira wanaelewa kuwa nafasi ya kiungo ndio muhimu kuliko nafasi nyingine uwanjani.Kama unavyojua tafsiri ya Kiswahili ya neno kiungo pia ndio hivyo hivyo tafsiri hiyo hutumika katika soka.Katika soka viungo ndio huunganisha mawasiliano kati ya mabeki na washambuliaji.Timu nzuri ni ile yenye viungo imara.Kwenye kiungo ndiko kwenye siri ya mafanikio.Madrid,Bayern,City na timu ya taifa ya Ujerumani wanaijua siri hiyo.Louis van gaal anajaribu kutuelewesha Darren fletcher ni mtu sahihi kwenye safu yake ya kiungo lakini garry monk na Gus poyet wametuonesha uongo wa Louis van gaal.Na kama kocha huyo ataendelea kuwa king’ang’anizi na stori yake ya fletcher na thom cleverely basi ategemee watu kuendelea kupiga miyayo na wakiichoka stori yake watamkimbiza kama hakukimbia mwenyewe. Manchester united imemsajili Angel di maria ambaye ni mchezaji bora wa real madrid nyuma ya Ronaldo na Bale lakini kiungo huyo si dawa ya gonjwa la united.Hapa van gaal anajaribu kusoma vizuri stori ya dokta wa muhimbili aliyemfanyia mgonjwa upasuaji wa kichwa baada ya mguu.Kama ni ukimwi di maria ni ARV.Ataongeza kitu katika timu ila hatatibu gonjwa la united.Manchester united inahitaji kiungo mkabaji mwenye roho ngumu mithili ya Nigel de Jong.Kiungo mwenye kariba ya de jong akisimama vizuri na ander Herrera hapo ndipo utaona makali ya Wayne rooney na van persie.Kwa sasa washambuliaji hao wanaonekana si lolote si chochote kwasababu ya atomi walizounganishwa nazo. Ukiacha kupwaya kwenye nafasi ya kiungo Manchester united imepwaya pia kwenye nafasi ya mabeki baada ya kuondokewa na wakongwe Nemanja vidic,Patrice evra na Ferdinand.Tegemeo pekee kwenye nafasi ya mabeki wa kati ni john evans na phil jones.Hapa napo van gaal inabidi apatazame kwa mapana na marefu kama anataka kuirudisha united ya sir alex ferguson. Manchester haina tatizo la washambuliaji wala viungo wasaidizi wa washambuliaji bali wana tatizo la Kiungo mkabaji na mchezeshaji sambamba na mabeki wa kati.Haihitaji vyeti kugundua matatizo hayo.Macho yangu hayahitaji kuvaa miwani na hasilani hayanidanganyi. Nakubali sina elimu ya ukocha kama van gaal ila hata yeye mwenyewe alikili kuwa timu yake haina uwiano mzuri(imekosa balance),wala siwezi ishi ndani ya kichwa cha van gaal kujua nini kapanga juu ya hatima ya Manchester united ila nnachoweza kumwambia au kumkumbusha van gaal ni kuwa kamwe hawezi kupika chapatti kwa unga wa muhogo.. Na Alleen kaijage 0655106767 kaijagejr@gmail.com

Posted via Blogaway

VAN GAAL HUWEZI KUPIKA CHAPATI KWA UNGA WA MUHOGO

Tunamshukuru aliyeleta wazo la kila kata kuwa na shule ya sekondari.Shule hizi kwa kiasi zimesaidia kufuta ujinga kwa walio wengi.Asilimia kubwa ya wanaomaliza shule za msingi wanapata nafasi za kuingia kidato cha kwanza tofauti na enzi zile za mwalimu na mzee wa ruksa.Heri nusu shari kuliko shari kamili,Ingawa shule hizi zina walakini lakini mchango wake kwenye jamii unaonekana.Tofauti ya sasa na zamani inaonekana kupitia shule hizi.Wengi hawajaelimika ila wamepunguza shari kwa kufuta ujinga.Wengi wao angalau wanajua kujieleza kwa lugha ya chakula,Pia wengi wanajua ukichanganya hydrogen na oxygen unapata maji,ukichukua sodium na chlorine unapata chumvi na ukitaka kupata chumvi na maji kwa pamoja ni lazima uchanganye acid na base. Hi ndio tunaita chemistry (kemia), kwa ufupi kemia ni masomo ya atomi na mkusanyo wa atomi kuwa molyekuli.Yaani hizo atomi ukizichanganya utapata kitu kizima kinachoitwa molyekuli,Hata ndugu zangu wajenzi wanajua ili upate zege lazima uchanganye ingredients(vitu vinavyounda zege),Ili upate zege lazima uchanganye maji, kokoto,mchanga na simenti kwa viwango maalumu. Kwenye soka tumekuwa tukitumia maneno kama chemistry (kemia) huku wengi tukiwa hatujui chimbuko lake.Mchezaji ndio atomi yenyewe na timu ndio molyekuli.Kitendo cha kuwaunganisha wachezaji katika timu moja na wachezaji hao kuungana katika mfumo husika ndio tunaita chemistry (kemia).Kocha anaposhindwa kupata wachezaji husika kwenye mfumo husika hapo ndipo tunasema kashindwa kutengeneza chemistry kwenye timu. Kocha wa manchester united Louis van gaal kama hakukimbia somo la chemistry basi anataka kutuonyesha staili mpya ya kupika chapati kwa unga wa muhogo.Van gaal amethubutu kutengeneza molyekuli ya 3-5-2 lakini amekosa atomi husika za kutengeneza chemistry.Watu wa mpira wanaelewa kuwa nafasi ya kiungo ndio muhimu kuliko nafasi nyingine uwanjani.Kama unavyojua tafsiri ya Kiswahili ya neno kiungo pia ndio hivyo hivyo tafsiri hiyo hutumika katika soka.Katika soka viungo ndio huunganisha mawasiliano kati ya mabeki na washambuliaji.Timu nzuri ni ile yenye viungo imara.Kwenye kiungo ndiko kwenye siri ya mafanikio.Madrid,Bayern,City na timu ya taifa ya Ujerumani wanaijua siri hiyo.Louis van gaal anajaribu kutuelewesha Darren fletcher ni mtu sahihi kwenye safu yake ya kiungo lakini garry monk na Gus poyet wametuonesha uongo wa Louis van gaal.Na kama kocha huyo ataendelea kuwa king’ang’anizi na stori yake ya fletcher na thom cleverely basi ategemee watu kuendelea kupiga miyayo na wakiichoka stori yake watamkimbiza kama hakukimbia mwenyewe. Manchester united imemsajili Angel di maria ambaye ni mchezaji bora wa real madrid nyuma ya Ronaldo na Bale lakini kiungo huyo si dawa ya gonjwa la united.Hapa van gaal anajaribu kusoma vizuri stori ya dokta wa muhimbili aliyemfanyia mgonjwa upasuaji wa kichwa baada ya mguu.Kama ni ukimwi di maria ni ARV.Ataongeza kitu katika timu ila hatatibu gonjwa la united.Manchester united inahitaji kiungo mkabaji mwenye roho ngumu mithili ya Nigel de Jong.Kiungo mwenye kariba ya de jong akisimama vizuri na ander Herrera hapo ndipo utaona makali ya Wayne rooney na van persie.Kwa sasa washambuliaji hao wanaonekana si lolote si chochote kwasababu ya atomi walizounganishwa nazo. Ukiacha kupwaya kwenye nafasi ya kiungo Manchester united imepwaya pia kwenye nafasi ya mabeki baada ya kuondokewa na wakongwe Nemanja vidic,Patrice evra na Ferdinand.Tegemeo pekee kwenye nafasi ya mabeki wa kati ni john evans na phil jones.Hapa napo van gaal inabidi apatazame kwa mapana na marefu kama anataka kuirudisha united ya sir alex ferguson. Manchester haina tatizo la washambuliaji wala viungo wasaidizi wa washambuliaji bali wana tatizo la Kiungo mkabaji na mchezeshaji sambamba na mabeki wa kati.Haihitaji vyeti kugundua matatizo hayo.Macho yangu hayahitaji kuvaa miwani na hasilani hayanidanganyi. Nakubali sina elimu ya ukocha kama van gaal ila hata yeye mwenyewe alikili kuwa timu yake haina uwiano mzuri(imekosa balance),wala siwezi ishi ndani ya kichwa cha van gaal kujua nini kapanga juu ya hatima ya Manchester united ila nnachoweza kumwambia au kumkumbusha van gaal ni kuwa kamwe hawezi kupika chapatti kwa unga wa muhogo.. Na Alleen kaijage 0655106767 kaijagejr@gmail.com

Posted via Blogaway

INAKUWAJE HADI MWANADADA MREMO KAMA HUYU ANAJIPIGA PICHA KAMA HIZI!!! UNADHANI ANAFIKIRIA NINI HAPO!!!

Sijui ni upweke au ndio mapozi ya kisasa...sasa
MUTOTO mzuri kama huyu KUJI-EXPOSE huko
FB ni haki kweli!!!

TAZAMA JINSI VIROBA VILIVYOMFANYA HUYU MWANADADA...VIPI UNAWEZA KUTOKANAYE AUTI DEMU KAMA HUYU?!!

 habari zingine  BOFYA HAPA 

"SYLVESTER STALLONE (RAMBO) AFARIKI BAADA YA AJALI MBAYA YA GARI" UVUMI WAENEA KWA HARAKA MIITANDAONI

Muigizaji wa the  "Expendables 3" Sylvester Stallone amekuwa mmoja wa mastaa wa Hollywood ambao wamekuwa ni waathirika wa kuzushiwa kifo. Tetesi zilizosambaa kama moto unaounguza pori/ msitu hasa hasa kupitia mitandao ya kijamii, zilianzia kupitia ukurasa feki wa facebook.

Habari hii ambayo inaonekana kusababisha panic kubwa kwa mashabiki wa muigizaji  "Rambo" imepelekea kutumwa kwa salamu za huzuni kutoka kwa mashabiki wake mbalimbali kupitia mtandao wa twitter.

Elinda Hagan @ElindaHagan
Follow

I just heard about Sylvester Stallone! Another favorite actor if mine, RIP

Ripoti hizo za
kifo cha Rambo zinadai kuwa alipata ajali mbaya ya gari iliyosababishwa
na  dereva wake aliekuwa amelewa na kutokuona gari kubwa lililokuwa
likija mbele yake.

Hii sio maara ya kwanza kwa muigizaji huyo kuuliwa na internet, mwanzoni uvumi mkubwa wa kifo chake ulioripotiwa na Global Associate News zilidai kuwa Rambo alifariki kwa ajali iliyotokana na snowboarding.

Sylvesta
Stallon (68) yuko hai na mwenye afya njema. Baada ya "Expendable 3"
atakuwa aki-shoot instalment ya 5 ya film yake "Rambo".

Ukiachana na Sylvester Stallon, wengine waliowahi kuzushiwa vifo ni pamoja na Justine Timberlake, Miley Cyrus na Charlie Hunnam

DUH!! NENO MOJA KWA HILI DENDA LA CHRIS BROWN NA DEMU WAKE MPYA KARRUECHE TRAN

HILI NDO CHEZAJI LA KIBRAZIL LINALOTARAJIWA KUINGIA BARCA HIVI KARIBUNI

KLABU ya Barcelona imekubali kumsajili beki wa kulia Douglas Pereira kutoka Sao Paulo kwa ada ya uhamisho ya Pauni Milioni 3.19, vigogo hao wa Katalumya wamethibitisha jana. Uhamisho unaweza kupanda kwa Pauni Milioni 1.2 zaidi kwa ajili ya beki huyo mwenye umri wa miaka 24 kulingana idadi ya mechi atakazocheza katika klabu yake mpya. Pereira atajiunga na klabu hiyo ya La Liga kwa mkataba wa miaka mitano iwapo atafaulu vipimo vya afya wiki hii nchini Hispania.

Hili ndo chezaji la wenger lililo ipiga shetani lekundu kipigo cha mbwa mwizi

Chezaji la Wenger: Mshambuliaji Benik Afobe anayecheza kwa mkopo MK Dons ya Daraja la Kwanza kutoka Arsenal, akishangilia bao la nne alilofunga jana dhidi ya Manchester United mchezo wa Kombe la Ligi. United ilichapwa 4-0, mchezaji huyo akifunga mabao mawili
Benik Afoba (kushoto) akifunga bao la tatu pembeni ya Keane wa United

New AUDIO | Stereo ft Victoria Kimani - Wako [Never Let You Down] | Download

TETESI ZA SOKA ZILIZOSHAMILI KWENYE MAGAZETI MBALIMBALI YA LEO JUMATANO ZIPO HAPA

Boss wa Manchester United Louis van Gaal anataka kumsajili kiungo wa Juventus Arturo Vidal, 27, kwa mkataba wa pauni milioni 34 kiasi ambacho kitafikisha pauni milioni 200 za kununua wachezaji Old Trafford katika kipindi cha miaka miwili (Independent), United huenda wakamtoa Javier Hernandez, 26, kwenda Juventus, katika mkataba wa Vidal (Daily Express), Manchester United pia wanatarajia kutaka kumsajili Daley Blind, 24 kutoka Ajax kwa pauni milioni 18 katika siku chache zijazo (Sun), Arsenal wanaonekana kuzidiwa kete na Roma, kumsajili beki wa kati Kostas Manolas, 23 kutoka Olympiakos (Goal), Manchester United na Arsenal wamepata matumaini ya kuendelea kumfuatilia beki wa Roma Mehdi Benatia, 27, baada ya klabu hiyo ya Italia kuvunja mazungumzo na Bayern Munich (Daily Star), Arsenal huenda wakamfuatilia Danny Welbeck, 23, kutoka Man United, au Loic Remy, 27, kutoka QPR kuziba pengo la Olivier Giroud ambaye huenda akakosa kucheza kwa miezi mitatu kutokana na jeraha la kiwiko cha mguu (Daily Telegraph), Southampton wameanza kumfuatilia beki wa Atletico Madrid Toby Alderweireld, 25, na kuwazidi Monaco (Times), Tottenham wapo tayari kutoa pauni milioni 8 kumchukua nahodha wa Sevilla Federico Fazio, 27 (London Evening Standard) Chelsea wanazungumza na Roma kumchukua Mattia Destro, 23 (Daily Mirror), QPR wanakaribia kumsajili beki wa Liverpool Jack Robinson, 20 kwa mkataba wa pauni milioni 1 (Daily Mirror), West Ham wamemuulizia beki wa kati wa Bayer Leverkusen Philipp Wollscheid, 25, (Daily Mail), Sunderland, QPR na West Brom wanamtaka kiungo wa Leicester Andy King, 25, (Sun), AC Milan bado wanataka kumchukua Fernando Torres kutoka Chelsea, wakala wake akipendekeza kumchukua kwa mkopo, ingawa mshahara wake mkubwa unaonekana kuwa kikwazo (Metro), Napoli wataanza kumfuatilia tena kiungo wa Tottenham, Sandro kwa mkopo (The Times), Sporting wamewaambia Arsenal kuwa watakubali kitita cha euro milioni 30 kumsajili William Carvalho, kama Arsenal watakubali kumtoa Serge Gnabry, Francis Coquelin au Yaya Sanogo kwa mkopo (The Times), Everton wanakaribia kukamilisha usajili wa Samuel Eto'o. Roberto Martinez alikuwa akimtaka Danny Welbeck wa Man United, lakini alikatishwa tamaa na bei ya Pauni milioni 15 (The Times) na boss wa Inter Milan, Walter Mazzarri amewaambia watu wake kuwa wako huru kujaribu kumsajili Ezequiel Lavezzi kutoka Paris St-Germain (Tuttosport). Zimesalia siku sita kabla ya dirisha la usajili kufungwa. Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Share hizi na wapenda soka wote