Thursday, September 18, 2014

UCL: Matokeo ya Man City vs Bayern Munich haya hapa

Ligi ya mabingwa wa ulaya imeendelea tena leo kwa michezo kadhaa kupigwa katika viwanja mbalimbali barani ulaya – kule Etihad stadium Manchester waliikaribisha FC Bayern Munich katika mchezo wa kundi E. Mchezo huo uliowakutanisha mabingwa wa ligi za Ujerumani na England ulikuwa mgumu na mpaka kufikia dakika ya 90 bado matokeo yalikuwa 0-0, sifa zimuendee Joe Hart wa City kwa umahiri wa kuokoa michomo ya washambuliaji wa Bayern. Katika dakika 3 za mwisho za nyongeza mchezaji wa zamani wa Man City – Jerome Boateng akaiadhibu timu yake ya zamani kwa kuifungia Bayern goli pekee na la ushindi kwenye mchezo huo. Boateng alifumu a shuti kali ambalo Hart alijaribu kulifuata lakini likamshinda na kuipa Bayern ushindi wa kwanza kwenye ambalo linahusisha vilabu vya Spartak na As Roma. Timu zilipangwa kama ifuatavyo: Bayern Munich: Neuer 7, Rafinha 6.5 (Pizarro. 84), Boateng 7, Benatia 6.5 (Dante, 85), Bernat 7.5, Lahm 6.5, Alonso 6.5, Alaba 7, Muller 6.5 (Robben, 76, 5.5), Lewandowski 6.5, Gotze 7 Subs: Reina, Dante, Shaqiri, Pizarro, Rode, Hojbjerg. Scorer: Boateng, 89. Manager: Pep Guardiola, 6.5 Man City: Hart 9, Sagna 6.5, Kompany 7, Demichelis 6.5, Clichy 6, Nasri 5.5 (Milner, 58, 6) Fernandinho 6, Toure 5.5, Navas 6 (Kolarov, 87), Silva 7.5, Dzeko 6 (Aguero, 74, 5.5) Subs: Caballero, Kolarov, Aguero, Lampard, Mangala, Boyata. Manager: Pellegrini, 6.5

Posted via Blogaway

0 comments:

Post a Comment