Monday, September 22, 2014
|
Mshambuliaji wa AS Roma ya
Italia, Alessandro Florenzi
amepiga bao na haraka
akapanda jukwaani na kwenda
kumkumbatia bibi mwenye
umri wa miaka 82.
Ilikuwa ni mechi kati ya AS
roma dhidi ya Cagliari na
wakashinda kwa mabao 2-0,
yote yakiwa yamepigwa na
mshambuliaji huyo.
Mara baada ya kufunga
mshambuliaji huyo alipanda
kasi kwenda juu ya jukwaa
na kumkumbatia bibi huyo.
Huo ulikuwa ni ushindi
mwingine wa AS Roma baada
ya kuwa imeiadhibu kwa
mabao 5-1 timu ya CSKA
Moscow katika Ligi ya
Mabingwa Ulaya. |
Posted via Blogaway
0 comments:
Post a Comment