Thursday, August 28, 2014

Q-Jay kusikika tena kwenye bongo fleva baada ya ukimya mrefu toka aokoke

Baada ya miaka kadhaa tangu mwimbaji wa R&B Joseph Kelvin Mapunda aka Q-Jay wa Wakali Kwanza kutangaza kuacha game ya bongo fleva, anatarajiwa kusikika tena kwenye muziki huo katika wimbo mpya. Q-Jay ni miongoni mwa wasanii watakaosikika kwenye wimbo mpya wa Dj Aaron unaotarajiwa kutoka Ijumaa (Agosti 29). Dj Aaron amewashirikisha Banana Zorro, Barnaba na Q- Jay katika wimbo huo uitwao ‘Peace One Day’, ambao ni wa kuhamasisha amani. Miaka kadhaa iliyopita Q-Jay aliyewahi kufanya vizuri na nyimbo kama ‘Sifai’, aliamua kuachana na muziki wa kidunia baada ya kuokoka na kutangaza kuwa atakuwa akifanya muziki wa gospel.

Ungana na familia ya habari kwa ku BOFYA HAPA 


Posted via Blogaway

0 comments:

Post a Comment