Thursday, August 14, 2014

Hutaamini ukiisikia sababu iliyomfanya Dogo Janja aache shule!

Rapper kutoka Arusha, Dogo Janja ameamua kuacha shule ili kusomea masomo ya muziki.

Akiongea na 255 ya kipindi cha XXL cha Clouds FM, Janjaro amedai kuwa usumbufualiokuwa akiupata shuleni ndio sababu kubwa iliyomfanya aache shule.

“Shule ambayo mimi nimesoma nilikuwa napata matatizo kwasababu kitu kidogo ambacho mnaweza mkafanya wote lakini wewe ukaonekana chanzo. ‘Msanii mhuni, huyu hivi,” alisema rapper huyo. “Sometimes unaweza ukawa unasoma watu wengi wako dirishani wanapita wanakuangalia. Au unaweza ukakosea.. yaani wanakuwa wewe ni mtu ambaye upo sahihi all the time.

Kwa mfano labda unajua zile za kushtukizwa ‘fulani jibu swali’ kila saa unaulizwa wewe,” aliongeza. “Kwahiyo unakuwa hakuna pale Uabdul, unakuwa unaweka Ujanjaro Udogojanja.

Kwasababu unajua ile kushtukizwa kila saa unakuwa unahisi kama mwalimu anakuandama sana. Au kwenye mtihani, mnaweza mkawa mnafanya wote mtihani lakini mwalimu anakuja kukusimamia wewe, anakukazia kinoma.” Nini mtazamo wako kuhusiana na sababu hiyo ya Dogo Janja iliyomfanya aache shule?

 ASANTE KWA KUTEMBELEA BLOG HII ILA TUNAOMBA SUPPORT YAKO KWA KUBONYEZA HAPA 

0 comments:

Post a Comment