| KOCHA wa Mafunzo ya Zanzibar, Hemed
Morocco, amesema kuwa kikosi cha Simba
kinaendelea kuimarika hasa safu ya viungo na
washambuliaji huku akidai bado kuna tatizo
kubwa katika safu ya mabeki hasa beki ya
pembeni.
Juzi Jumatano Mafunzo ilicheza na Simba katika
Uwanja wa Amaan ambapo iliambulia kipigo
cha mabao 2-0 ila kocha huyo alidai kuwa
alikuwa anakiangalia tu kikosi chake kwani
bado hajaanza kazi rasmi.
Morocco alisema kuwa Simba wana timu nzuri
ila kocha Patrick Phiri anatakiwa kufanya
marekebisho haraka hasa nafasi hiyo ili isije
ikamgharimu katika mechi za Ligi Kuu Bara
msimu ujao.
“Ukiiangalia Simba ya sasa ni tofauti na ya
msimu uliopita, nafasi ya kati na mbele
wanacheza sana kwa kuelewana na wapo vizuri
kuliko nafasi ya nyuma, sasa hilo ni tatizo
ambalo kocha anatakiwa kulirekebisha,”
alisema.
“Kwa upande wa timu yangu ni vigumu
kuzungumzia mapungufu yake kwani katika
mechi hiyo nilikuwa naangalia tu kazi ya
kuifundisha timu hiyo inaanza rasmi wiki ijayo,
lakini kikubwa nampongeza Phiri kwa
kuitengeneza upya Simba.”
Katika mechi hiyo ya kirafiki, safu ya
ushambuliaji ya Simba iliongozwa na Amissi
Tambwe pamoja na Shaban Kisiga ambaye pia
anacheza nafasi ya kiungo.
Viungo ni Amri Kiemba, Pierre Kwizera,
Ramadhan Singano ‘Messi’ na Haruni Chanongo
huku mabeki akiwatumia Issah Rashid ‘Baba
Ubaya’, Joseph Owino, Joram Mgeveke, William
Lucian ‘Gallas’ huku golini akisimama Ivo
Mapunda.credit mwanaspoti |
0 comments:
Post a Comment