Sunday, September 21, 2014

DUNIA IMEKWISHA: LIVE..MTOTO WA MCHUNGAJI, BINTI MWANAKWAYA KANISANI WANASWA KICHAKANI

Wanakwaya wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God, Hanipher na Godfrey (mtoto wa mchungaji) walionaswa wakiwa kichakani. kama nimeokooka, utantambuaje kama namuheshimu Mungu…” Wimbo huu wa Injili ulioimbwa na Bony Mwaitege wengi hupenda kuusikiliza kama burudani lakini una ujumbe mzito hasa kwa wale wanaosema wameokoka.Hivi karibuni mjini Iringa, wanakwaya wawili wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God, mwanamke alijitambulisha kwa jina moja la Hanipher na mwanaume aliyesema anaitwa Godfrey, walinaswa usiku kichakani katika mazingira yaliyojaa utata, Risasi Jumamosi linakupa kisa kamili. Tukio hilo la kushangaza, lilijiri kwenye eneo la Makanyagio ambalo lina makaburi ya awali katika Manispaa ya Iringa licha ya kuwepo na nyumba za wenyeji pia. Kwa mujibu wa chanzo chetu, wanakwaya hao walinaswa na sungusungu ambao siku za hivi karibuni wamekuwa wakifanya ‘patroo’ katika eneo hilo na la Isoka kufuatia kuwepo kwa matukio ya wakazi wake kuvamiwa, kupigwa na kuporwa mali. Siku ya tukio, sungusungu hao wakiwa katika majukumu yao waliwaona wanakwaya hao wakiacha njia kuu na kuchepukia porini umbali unaokadiriwa kuwa mita 20 kutoka barabarani. “Ilibidi sungusungu wawafuate hadi kule kichakani, ndipo walipowakuta katika mazingira tata na yenye maswali mengi bila majibu. Mbaya zaidi, yule mwanamke alikuwa na mtoto wa mwaka mmoja mgongoni,” kilisema chanzo chetu.BOFYA APO CHINI KUSOMA ZAIDI>>

 BOFYA HAPA  

null

0 comments:

Post a Comment