Saturday, August 23, 2014
 |
KOCHA mwenye heshima kubwa
ndani ya Simba na ambaye
amekabidhiwa jukumu la
kuiongoza timu hiyo msimu ujao,
Mzambia Patrick Phiri, ametumia
Mwanaspoti kuwaambia mashabiki
wa timu hiyo kwamba washushe
pumzi mambo ni mazuri.
Amewasisitiza kwamba wasiwe na
wasiwasi kwa vile kila kitu kipo
sawa na heshima lazima irudi
Msimbazi kwani ratiba ya Ligi Kuu
Bara ameshaipata na wala
haimsumbui.
Katika mazoezi ya jana Ijumaa
yaliyofanyika Uwanja wa Chuoni
Chukwani, Phiri alisema wachezaji
wake wanapokea kwa kiasi
kikubwa mafunzo yake na
anapenda kuona wanavyomiliki
mipira, kukaba na kushambulia.
Alichofanya jana ni kuwapunguzia
muda wa mazoezi ambayo awali
alikuwa akitumia saa nne na sasa
anatumia saa tatu ili wapate muda
wa kutafsiri mafunzo yake kambini
na kutuliza akili.
“Nafurahi kwa sababu naona
wachezaji wananielewa kila
ninachokihitaji, inanipa moyo sana
kwamba msimu ujao tutafanya
vizuri, nimetumia muda mwingi
kuwafundisha jinsi ya kumiliki
mipira, kukaba na kushambulia,
kesho (leo Jumamosi) watafanya
kidogo tu ili mwili ukae sawa tayari
kwa mechi ya Jumapili dhidi ya
Kilimani City (ya Daraja la Pili
Zanzibar),” alisema Phiri.
Akizungumzia maandalizi yake ya
Ligi Kuu, alisema kuwa ameiona
ratiba na mpangilio wake ni mzuri
kwani watacheza mechi nyingi
nyumbani katika mzunguko wa
kwanza ila amesisitiza mechi yenye
presha kuwa ni dhidi ya Yanga
itakayochezwa Oktoba 12 Uwanja
wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
“Ratiba imepangwa vizuri,
tunatakiwa kushinda mechi zote
lakini kwa uelewa wangu katika Ligi
hii ya Tanzania mechi ya Yanga ina
presha kubwa kwani ina mambo
mengi sana hata kabla ya mechi
kuchezwa, lakini tutajipanga
kuhakikisha tunafanya vizuri,”
alisema Phiri.
AMCHEZEA AKILI MAXIMO
Katika kile ambacho ni kuonekana
kumchezea akili kocha wa Yanga,
Marcio Maximo, kama
wanavyofanya makocha mahiri wa
Ulaya, Phiri amedai kukerwa na
ujio wa Yanga mjini Unguja.
Yanga ilikuwa kambini Pemba
lakini leo Jumamosi inatua Unguja
na Kesho itacheza na KMKM
kwenye Uwanja wa Amani.
Phiri amedai hajafurahia Yanga
kuamua kucheza mechi hiyo dhidi
ya KMKM siku ambayo wao wana
mechi katika uwanja huo wa
Amani, mechi ya Yanga itaanza saa
10:00 jioni wakati ya Simba itaanza
saa 2:30 usiku dhidi ya Kilimani.
Phiri aliliambia Mwanaspoti
kwenye kambi ya timu hiyo mjini
hapa akisema: “Najaribu kuangalia
itakuwaje kwani sisi ndio tumeanza
kuja hapa na kutoa taarifa kuwa
siku ya Jumapili tutakuwa na
mechi, iweje Yanga nao wanataka
wacheze siku hiyo hiyo? Kama
uwanja usingekuwa mmoja hapo
sawa, lakini nao wanataka kucheza
uwanja ambao tutautumia.Credit mwanaspoti |
Habari zingine za michezo BONYA HAPA
0 comments:
Post a Comment