Tuesday, September 30, 2014
 |
| Kocha wa Chelsea, Jose
Mourinho haishi vituko,
lakini safari hii
alikutana na kali zaidi.
Katika mechi ya Ligi Kuu
England dhidi ya Aston
Villa, wakati Chelsea
inaongoza kwa mabao 3-0,
zikiwa zimebaki dakika
chache kabla ya mechi
kwisha, akainuka na kwenda
kwenye benchi ka Aston
Villa na kutaka kuwapa
mkono makocha.
Kocha Mkuu, Paul Lambert
kwanza akagoma na kuhoji
muda ulikuwa bado, baadaye
akatoa mkono kishikaji.
Lakini msaidizi wake, Roy
Keane wala hakuwa na
habari, wakati Mourinho
anampa mkono, yeye
akaendelea kuangalia
mechi.
Mourinho akajitahidi
kumgonga begani, Keane
akaendelea kuuchupua na
Mourinho akachukua zake
time. |
0 comments:
Post a Comment